Hussein Machozi - Kafia Ghetto (Official Audio)
Hussein Machozi Hussein Machozi
75.1K subscribers
18,879 views
0

 Published On Premiered Apr 19, 2021

Siku nyingi binti namfukuzia
Alishantosa nishakata tamaa
Sikujua kama kwangu angekuja
Nilitoa matumaini ya kumpata
Siku nyingi binti namfukuzia
Alishantosa nishakata tamaa
Sikujua kama kwangu angekuja
Nilitoa matumaini ya kumpata
(Leo hii kaja mwenyewe mchumba)
Ghetto kwangu mpaka ndani kaingia
(Nilimuuliza naeza kukusaidia)
Akacheka kisha akaniambia
Ombi langu lile amenikubalia
Siku zote alikuwa akinifikiria
Niliruka kwa furaha kubwa sana
Sikuamini kama mchumba ningempata

(Usilojua ni usiku wa giza)
Ningetambua bora ningemtimua
(Usilojua ni usiku wa giza)
Ningetambua bora ningemtimua

Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?

Baada ya stori binti nilimuuliza
Kinywaji gani angeweza kutumia
Alinieleza kisha mi nikainuka
Nikaelekea dukani kununua
Baada ya stori binti nilimuuliza
Kinywaji gani angeweza kutumia
Alinieleza kisha mi nikainuka
Nikaelekea dukani kununua
(Huwezi amini nyuma nilipomuacha)
Baada ya kurudi ndipo kizaa zaa
(Binti alikuwa kitandani kajilaza)
Nilimuamsha lakini hakuamka
Pumzi zake zilikuwa zimekata
Nilidhani labda kazimia
Maji ya baridi kichwani nilimwagia
Lakini hata hakushtuka
(Kumbe alikuwa tayari ameshakufa)
Nimekwisha Hussein bila kujua
(Kumbe alikuwa tayari ameshakufa)
Nimekwisha Machozi bila kujua

Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?

Ee Mola, nimekosa nini?
Ee Mola, niokoe mimi
Ee Mola basi nipe akili
Mimi nifanye nini
Ee Mola, nimekosa nini?
Ee Mola, niokoe mimi
Ee Mola basi nipe akili
Mimi nifanye nini
Furaha yangu, imekuwa kilio changu (kilio changu)
Furaha yangu, imekuwa kilio changu
Ndoto zangu leo majonzi kwangu
Ntawaeleza nini walimwengu?
Ndoto zangu leo majonzi kwangu
Ntawaeleza nini walimwengu?
(Vipi, wataniona mi ni mkweli?)
(Vipi nikiwaelezea wataniamini?)
(Vipi, wataniona sio katili?)
(Vipi, ingekuwa wewe ungefanya nini?)

Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?
Nani, ataniona mi ni mkweli?
Nani nikimuelezea ataniamini?
Nani, ataniona sio katili?
Nani, atanisaidia mimi?

Subscribe For More Official Content From Hussein Machozi: https://m.youtube.com/c/HusseinMachoz...

Hussein Machozi Booking Info:
Email: [email protected]

Catch Up With Hussein Machozi On:
Instagram:   / husseinmachozi100  
Twitter:   / machozihussein  

Listen To Hussein Machozi:
Apple Music:   / hussein-machozi  
Spotify: https://open.spotify.com/artist/20okz...
AudioMack: https://audiomack.com/hussein-machozi
Boomplay: https://www.boomplay.com/share/artist... srModel=COPYLINK&srList=IOS
Mdundo: https://mdundo.com/a/234831

show more

Share/Embed