Published On Premiered Jun 20, 2024
DODOMA: Mbunge wa Viti Maalum, Ester Bulaya amesema sababu ya Serikali kushusha kiwango cha malipo ya mkupuo kwa wastaafu ni kutumia fedha toka kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kuwekeza katika miradi ambayo hairejeshi fedha hizo.
Bulaya amesema hayo wakati akichangia bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka 2024/25 pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2024/25, bungeni jijini Dodoma.
Amehoji kama Serikali inaamini kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii iko vizuri, kwanini inashindwa kuwapa wafanyakazi uhuru wa kuchagua kiwango cha malipo ya mkupuo ambacho wanataka kulipwa?
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: https://instagram.com/habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: https://instagram.com/spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: https://twitter.com/HabariLeo?s=09