LIVE: DAY1: KAHAMA NET EVENT YATOSHA JANGWANI
MANUMBU TVπŸŒπŸ“š MANUMBU TVπŸŒπŸ“š
647 subscribers
56 views
2

 Published On May 12, 2024

MHUDUMU: MCH, MAGULILO MWAKALONGE.
*HOTUBA KUU JIONI.11/05/2024
SOMO: YATOSHA JANGWANI.
Mikutano hii ni mitakatifu ya Mungu kwa ajili ya kututoa na kutuleta katika amani pamoja na Kristo hivyo kukaa Jangwani imetosha.
Jangwa ni nini? Ni kiwakilishi cha dhambi, dhiki, mateso ndiyo maana tunapaswa kutoka huko na kurudi kwa Yesu. Swali la msingi ni hili, ni nani alitupeleka huko? Tuliingiaje huko? Nini chanzo cha asili cha kuwepo huko? Dunia inakumbwa na mafuriko, vita, kukosa amani. Lakini nini chanzo? Nani mama yao? Jibu ni hili chanzo Ni DHAMBI.
Kuna vielelezo vingi vya maisha na safari Jangwani. Na kielelezo kimojawapo ni safari ya Wana wa Israeli kutoka Misri kwenda Kanaani. Kulikuwa na njia fupi na ndefu ambapo ile ndefu ilikuwa umbali wa km 623-630, na ile fupi ni km 400, Ndiyo maana wakaingia huko Jangwani
Hakika yangu hamtaingia ninyi katika nchi, ambayo niliinua mkono wangu ya kwamba nitawaketisha humo, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni. Kwa hesabu ya hizo siku mlizoipeleleza ile nchi, yaani, siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka, mtayachukua maovu yenu, ndiyo miaka arobaini, nanyi mtakujua kufarikana kwangu. Mimi Bwana nimekwisha nena, hakika yangu ndilo nitakaloutenda mkutano mwovu huu wote, waliokusanyika juu yangu; wataangamia katika nyika hii, nako ndiko Watakakokufa. Kisha hao watu, ambao Musa aliwatuma waipeleleze nchi, waliorudi, na kufanya mkutano wote kumnung'unikia, kwa walivyoleta habari mbaya juu ya nchi, watu hao walioileta habari mbaya ya nchi wakafa kwa tauni mbele ya Bwana. Hesabu 14:30-37.
Adamu na Hawa ndiyo walikaribishiwa duniani ikiwa mpya kabisa lakini wakadanganywa na yeye akaukataa ukweli wa Mungu na kuukubali uongo wa Shetani. Majangwa huwa yanaanzia kwa kumkataa Mungu na hivyo Adamu na Hawa wakaanguka.
Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake. Mathayo 13:24-25

Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. Ezekieli 28:15

Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa! Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu. Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo. Wao wakuonao watakukazia macho, Watakuangalia sana, wakisema, Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, Huyu ndiye aliyetikisa falme; Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake; Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao? Isaya 14:12-17

Ndiyo unabii ukatimia ulivyotimia katika pambano na ulitimia hivi;

Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. Ufunuo wa Yohana 12:7-9

Hivyo ndivyo chanzo cha Jangwa kilivyoanza. Ila katika vita hii Shetani hakushinda kabisa alishindwa mbinguni akatupwa duniani.

Uzinzi hauji peke yake, hata uongo hauji peke yake ndiyo maana dhambi inaharibu urafiki kati ya Mungu na Mwanadamu.

Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini. Kumbukumbu la Torati 2:3.

Yesu angekuwa amaeshakuja lakini watu bado wamemng'ang'ania sana shetani, hivyo tunamchelewesha Yesu kuja kwa sababu bado tuko katika Jangwa.

Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. Yohana 10:10.

Hakika imetosha jangwani turudi kwa Yesu maana Yeye ndiye alikuja kutupatia Uzima, yatoshwa jangwani.

Yesu anahitaji kututoa Jangwani kwakuwa katika Neno lake anasema;

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16

Mkimbilie Yesu na shetani atawakimbia.

Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Yakobo 4:7

192-Mwamba Wenye Imara
Rock Of Ages (SDA300)
Doh ni C

Mwamba wenye imara Kwako nitajificha!
Maji haya na damu Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi, Hunifanya mshindi.

Kwa kazi zote pia Sitimizi sheria.
Nijapofanya bidii, Nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa; Ndiwe wa kuokoa.

Sina cha mkononi, Naja msalabani;
Nili tupu, nivike; Ni mnyonge, nishike;
Nili mchafu naja, Nioshe nisijafa.

Nikungojapo chini, Na kwenda kaburini;
Nipaapo mbinguni, Na kukwona enzini,
Roho yangu na iwe Rahani mwako wewe.
#channel #citizentv #global #efmedia #itv #kitengetv #manara #tanzania #tbc
cc#Manumbutv

show more

Share/Embed