Published On Sep 29, 2024
Wananchi wametakiwa kutekeleza wajibu wao wa kisheria wa kusafisha Mazingira ili wapate haki ya kuishi katika sehemu safi na salama kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha sheria ya usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004
Hayo yamejiri wakati wa zoezi la usafishaji Fukwe za Bichi ulioratibiwa na Taasisi ya Utu na Mazingira HUDEFO na kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwepo Ubalozi wa Ireland Tanzania ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Sarah Pima amesema utupaji wa taka Baharini ni mkubwa hivyo jitahada za Pamoja zinahitajika ili kuikabili hali hiyo
Naye Meneja kanda ya Temeke kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC Anold Mapinduzi amewataka wananchi kila mmoja kusafisha Mazingira yake na kuacha kuzalisha taka ambazo sio lazima kuzalisha