MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"
Global TV  Online Global TV Online
4.91M subscribers
46,067 views
0

 Published On Streamed live on Apr 13, 2018

MAKONDA: "Endeleeni Kunitukana, ila Ukiitwa Kimbia Usisubiri Nikufate"

NI wiki ya kitimtim! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutoa wito kwa wanawake waliotelekezewa watoto na wanaume kufika ofisini kwake, Ilala jijini Dar kwa ajili kupatiwa msaada wa kisheria.

Awali, zoezi hilo lililotarajiwa kudumu kwa takriban siku 5 mfululizo, lilianza kuchukua nafasi Jumatatu iliyopita ambapo mamia ya wanawake walijitokeza na kuifanya ofisi ya mkuu wa mkoa kufurika, hadi kufikia hatua ya kuzuia kwa muda safari za magari katika njia ambazo zinakutana katika ofisi hiyo.

Wanawake wasiopungua 480 walijitokeza ambapo kwa mujibu wa Makonda, 47 kati yao waliwataja waheshimiwa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku 14 wakiwa ni viongozi wa dini.

Akizungumza na wanahabari mara baada ya wanawake wengi kujitokeza na kusikilizwa na wanasheria mbalimbali pamoja na watu wa dawati la jinsia, Makonda alitoa wito kwa wanaume ambao wametajwa na wanawake wao waliowatelekeza, wajitokeze wenyewe ili kusikiliza kesi zao. Makonda alienda mbali zaidi kwa kuwataka wanaume ambao nao wametelekezewa watoto au wenye malalamiko mbalimbali dhidi ya wanawake, nao wafike ofisini kwake kwa ajili ya kusaidiwa.

WANAUME NAO WAJITOKEZA

Mara baada ya Makonda kutoa wito huo, Jumanne iliyopita wanaume walijitokeza katika ofisi yake na kutoa malalamiko mbalimbali.

Kuna ambao walidai kukimbiwa na wanawake wao kutokana na kuugua kwa muda mrefu, kuna wengine walilalamikia wake zao kugeuza nyumba kuwa danguro. Kama hiyo haitoshi, kuna mpiga picha maarufu wa Ilala jijini Dar, Vedasto Mdesa ambaye alisema amefika ofisini hapo ili kueleza jinsi alivyokimbiwa na mkewe.

“Mimi na mke wangu tulibahatika kuzaa watoto watatu, wawili wakiwa mapacha, mke wangu niliyezaa naye tulikutana hapa mjini akisoma Chuo Cha Kampala University na tulikuwa tunapendana lakini familia yake ndiyo haikukubali mimi kumuoa mwanamke huyo.

“Nimekuwa nikipata shida sana ya kukutana na mzazi mwenzangu kutokana na uchumi wangu kuwa mdogo kwani mimi ni mpigapicha tu eneo la Buguruni, nimekuwa nikipata vikwazo vingi kutokana na familia yangu kuwa ya kimaskini na mke wangu kutoka katika familia ya kitajiri, kiukweli mke wangu yeye anatoka familia ya kitajiri na ndugu zake wengine wanaishi Urusi na ndiyo hasa wanaosababisha mimi nisiishi na huyo mwanamke lakini bado nampenda na yeye ananipenda, cha msingi namuomba Makonda anisaidie niweze kurudishiwa familia yangu,” alisema paparazi huyo.

WATU WAKESHA

Kuonesha kwamba tatizo hilo ni kubwa, usiku wa kuamkia Jumatano, wapo akinamama ambao walidaiwa kukesha katika ofisi ya Makonda ili kuweza kuwahi foleni asubuhi na mapema.


lnstal GlobalPublishersApp Android: http://bit.ly/2AAQe1d iOS: http://apple.co/2Assf4M Subscribe    / uwazi   FACEBOOK:   / globalpublis.  .

TWITTER:   / globalhabari   Visit https://globalpublishers.co.tz/, Subscribe    / uwazi1  

kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya…    / uwazi1      / uwazi1      / uwazi1   WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK:   / globalpublis.  . TWITTER:   / globalhabari   INSTAGRAM:   / globalpubli  .

show more

Share/Embed