Masoud Kipanya: Kwanini sitaogopa kumchora Rais (NYUNDO YA BARUAN MUHUZA - 17/01/2019)
Azam TV Azam TV
2.75M subscribers
248,718 views
1.4K

 Published On Jan 17, 2019

Mchoraji wa katuni maarufu ya ‘Kipanya’, ambaye pia ni mtangazaji wa radio na TV, Masoud Kipanya amefunguka kuwa hajawahi kuogopa kumchora kiongozi mkuu wa nchi (Rais) kwa kuwa havunji sheria yoyote.

Masoud ameeleza hayo katika kipindi hiki cha Nyundo ya Baruan Muhuza kilichoruka Alhamisi ya tarehe 17/01/2019 baada ya kuulizwa swali hilo na mtangazaji, Baruan Muhuza.

Mbali na hilo, Masoud amezungumza mengi ikiwemo historia yake katika uchoraji na utangazaji, jinsi alivyoajiriwa kisha kufukuzwa kazi katika Kituo cha Radio cha Clouds FM na jinsi alivyorejea kazini baada ya kukaa nje ya kituo hicho kwa muda wa miaka nane, ilipofia biashara yake ya mavazi ya KP Wear n.k.

Mengine aliyoyaweka wazi ni kiini cha ugomvi wake na aliyekuwa mtangazaji mwenzake waliyekuwa naye Clouds FM, Gerald Hando, story ya yeye kupotea iliyomtokea mwanzoni mwa mwaka jana 2018 n.k.

Pia amemtaja mtu aliyempa jina la Kipanya.

Kipindi cha #NyundoYaBaruanMuhuza ni kila Alhamisi saa 1:00 usiku #AzamSports2

show more

Share/Embed