Published On Premiered Apr 12, 2021
Mtoto Charles Mathias mwenye umri wa miaka 6 alijizolea umaarufu mitandaoni mwezi February kutokana na kipaji chake cha kuhesabu akiwa katika kijiji cha Nyigwa kata ya kibungo juu wilaya ya Morogoro Vijijini. Baada ya kuonyesha uwezo wake huo wa hesabu wengi walijitokeza kila mmoja akitaka kuwa sehemu ya kukiendeleza kipaji cha mtoto huyu.
Hatimaye leo mtoto Charles Mathias ameanza masomo yake kwenye shule ya Fountain Gate iliyopo jijini Dodoma.Shule hiyo itakuwa na jukumu la kuratibu na kumuendeleza, elimu ya msingi hadi elimu ya juu pamoja na kusimamia makuzi ya kimwili na kiroho.
show more